Isaiah 27:1-6
Wokovu Kwa Ajili Ya Israeli
1 aKatika siku ile, Bwana ataadhibu kwa upanga wake,upanga wake mkali, mkubwa na wenye nguvu,
ataadhibu Lewiathani ▼
▼ Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa.
yule nyoka apitaye kwa mwendo laini,Lewiathani yule nyoka mwenye kujipinda;
atamuua joka huyo mkubwa sana wa baharini.
2 cKatika siku ile: “Imbeni kuhusu shamba la mizabibu lililozaa:
3 dMimi, Bwana, ninalitunza,
nalinyweshea maji mfululizo.
Ninalichunga usiku na mchana
ili mtu yeyote asije akalidhuru.
4 eMimi sijakasirika.
Licha pangekuwepo michongoma na miiba kunikabili!
Ningepambana dhidi yake katika vita,
ningeliichoma moto yote.
5 fAu niwaache waje kwangu kwa ajili ya kupata kimbilio,
wao na wafanye amani nami,
naam, wafanye amani nami.”
6 gKatika siku zijazo, Yakobo atatia mizizi,
Israeli atatoa chipukizi na kuchanua maua,
naye atajaza ulimwengu wote kwa matunda.
Copyright information for
SwhKC